Majina ya Walimu

OFISI YA RAIS

SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA

15/10/2024

Kumb.Na.AB.113/388/01/25

TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI

Katibu wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa niaba ya MDAs & LGAs anapenda

kuwataarifu Waombaji Kazi wote walioomba kazi kuwa usaili unatarajiwa kuendeshwa kuanzia

tarehe 23/10/2024 hadi 16/11/2024 hatimaye kuwapangia vituo vya kazi waombaji kazi watakaofaulu

usaili huo.Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-

1. Usaili utafanyika kuanzia tarehe kama ilivyooneshwa kwenye tangazo hili muda na sehemu

ambapo usaili utafanyika umeainishwa kwa kila Kada.

2. Kila msailiwa anatakiwa kufika kwenye eneo la usaili akiwa amevaa Barakoa (Mask)

3. Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;

4. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga

kura,Kitambulisho cha kazi,Kitambulisho cha Uraia, Hati ya kusafiria, Leseni ya Udereva au barua

ya utambulisho kutoka Serikali ya Mtaa/Kijiji unachotoka.

5. Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa,kidato cha IV,

VI, Astashahada, Stashahada,Stashahada ya Juu, Shahada na kuendelea kutegemeana na

sifa za Mwombaji.

6. Wasailiwa watakaowasilisha Testimonials, Provisional Results, Statement of results, hatiza

matokeo za kidato cha IV na VI (form V and form VI results slips) HAVITAKUBALIWA NA

HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI.

7. Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi.

8. Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili.

9. Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa

na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA)

10. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakukidhi

vigezo. Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji

ya tangazo husika.

11. Kwa kada ambazo wanatakiwa kusajiliwa na Bodi zao za Kitaaluma wanapaswa kuja na vyeti

vyao Halisi vya Usajili pamoja na Leseni za kufanyia kazi.

12. Wasailiwa wote walioitwa kwenye usaili wahakikishe wanaingia kwenye akaunti zao na kunakili

namba ya mtihani kwa kuwa namba hizo hazitatolewa iku ya usaili.

 

 

 

MWAJIRI: MDAS & LGAS

KADA: MWALIMU DARAJA LA III A – ELIMU YA AWALI

TAREHE YA USAILI WA MCHUJO:Oct. 23, 2024, 7 a.m.

MAHALI:

USAILI HUU UTAFANYIKA KATIKA VITUO MBALIMBALI KULINGANA NA ANUANI YA MUOMBAJI YA SASA (CURRENT

RESIDENT REGION) KWA TAARIFA ZAIDI TEMBELEA TOVUTI YA SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA.

TAREHE YA USAILI WA MAHOJIANO:Nov. 16, 2024, 7 a.m.

MAHALI:

USAILI HUU UTAFANYIKA KATIKA MKOA AMBAO MSAILIWA ALICHAGUA NA KUTHIBITISHA KUWA AMEOMBA KAZI KATIKA

MKOA HUO. KITUO CHA USAILI UTAJULISHWA KUPITIA AKAUNTI YAKO YA AJIRA PORTAL NA TOVUTI YA SEKRETARIETI

YA AJIRA (www.ajira.go.tz).

 

 

 

See attachment Bellow.

20241510072349MWALIMU DARAJA LA IIIA -23-10-2024